Monday, January 18, 2016

UNITED YAMUWANIA SANCHEZ.

KLABU ya Manchester United, imeripotiwa kumuwania chipukizi wa Benfica, Renato Sanchez. Chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 18, amekuwa akionyesha kiwango cha juu toka alipoibuka katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo na sasa amekuwa akifuatiliwa na vilabu kadhaa barani Ulaya vikiwemo Newcastle United, Swansea City na Aston Villa. Taarifa zaidi zinadai kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Ureno ambaye ana mkataba unaomalizika mwaka 2020 ana thamani ya paundi milioni 58.8 kwa klabu itakayomuhitaji. Pamoja na hayo United inatajwa kumuwania ingawa haikuwekwa wazi kama watamuhitaji kipindi cha Januari au Kiangazi.

No comments:

Post a Comment