Monday, February 22, 2016

BRAZIL WAFURAHIA KUNDI WALILOPANGWA COPA AMERIKA.

MKURUGENZI wa ufundi wa Shirikisho la Soka la Brazil, Gilmar Rinaldi amesema amefurahishwa na kundi walilopangwa katika michuano ya Copa America mwaka huu. Brazil ambao ni mabingwa mara nane wa michuano hiyo wamepangwa kundi B sambamba na timu za Ecuador, Haiti na Peru katika ratiba iliyopangwa jijini New York, Marekani jana. Akihojiwa mara baada ya upangwaji wa ratiba hiyo, Rinaldi amesema imekuwa ahueni kwao kwani wamepangwa kundi ambalo kidogo lina afadhali kulinganisha na mengine. Akizichambua timu walizopangwa nazo, Rinaldi amesema Ecuador kwasasa wanapitia kipindi kizuri kwani wanaongoza katika kundi katika mechi za kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2018 hivyo ni timu yenye ushindani na wanapaswa kuwa heshimu. Rinaldi aliendelea kudai kuwa Peru walikuwa wakisuasua katika michuano hiyo iliyofanyika mwaka jana lakini tayari wameimarika. Mkurugenzi huyo amesema Haiti hawaifahamu sana hivyo watatuma wawakilishi wao kwenda kuipeleleza ili waweze kujiandaa vyema pindi watakapokutana nao.

No comments:

Post a Comment