Monday, February 22, 2016

MCHEZAJI ATOLEWA NJE BADA YA KUMUONYESHA MWAMUZI KADI NYEKUNDU.

MCHEZAJI wa klabu ya Trabzonspor, Salih Dursun ametolewa nje kwa kumuonyesha mwamuzi kadi nyekundu wakati wa mchezo waliofungwa mabao 2-1 na Galatasaray katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uturuki uliofanyika jana. Tukio hilo lilitokea dakika ya 86 ya mchezo baada ya mwamuzi Denis Bitnel kumuonyesha kadi nyekundu ya moja kwa moja Luis Cavanda kwa kufanya madhambi ndani ya eneo la hatari. Wachezaji wa Trabzospor walimzonga mwamuzi kupinga kadi hiyo ambapo Dursun alimnyang’anya mwamuzi kadi aliyokuwa nayo na kumuonyeshea hatua ambayo ilipelekea na yeye kutolewa hivyo kuwafanya wenzake kucheza pungufu zaidi. Hii sio mara ya kwanza kwa klabu hiyo kuingia katika mizozo na waamuzi, kwani Novemba mwaka jana mwenyekiti wao Ibrahim Haciosmanoglu alifungiwa siku 280 baada ya kuwafungia waamuzi wanne uwanjani kwa kushindwa kutoa penati kwa timu hiyo.

No comments:

Post a Comment