Wednesday, February 24, 2016

MOURINHO AKANUSHA TETESI ZA KWENDA UNITED.

MENEJA wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho amesema hafahamu kuhusu yeye kuja kuwa meneja ajaye wa Manchester United lakini ana matumaini ya kurejea katika soka majira ya kiangazi. Mapema mwezi huu, taarifa zilizagaa kuwa United walikuwa wamefanya mazungumzo na wawakilishi wa meneja huyo raia wa Ureno. Mourinho mwenye umri wa miaka 53, alitimuliwa na Chelsea Desemba mwaka jana ikiwa imepita miezi saba toka atwae taji la Ligi Kuu. Akijibu swali la mwana habari wakati akiwa katika shughuli za kijamii huko Singapore, Mourinho amesema hafamu lolote kuhusu yeye kuja kuwa meneja wa United lakini anachofahamu yeye ni kuwa atarejea katika masuala ya soka ifikapo majira ya kiangazi.

No comments:

Post a Comment