Wednesday, February 24, 2016

RONALDO NDIO MFALME WA MITANDAO YA KIJAMII, AFIKISHA MASHABIKI MILIONI 200.

MSHAMBULIAJI nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo ameweka historia katika mitandao ya kijamii kufuatia kuwa mwanamichezo wa kwanza kufikia idadi ya watu milioni 200 wanaomfuatilia katika mitandao ya Facebook, Instagram na Twitter. Ronaldo ana mashabiki milioni 109.7 wanaomfuatilia katika Facebook, milioni 49.6 wanaomfuatilia katika Instagram na milioni 40.7 wanaomfuatilia katika Twitter. Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno sasa wanakuwa na mashabiki wengi wanaomfuatilia katika mitandao hiyo kuliko wanamichezo wengine wa zamani na wa sasa wakiemo nyota wa zamani wa NBA Michael Jordan, Kobe Bryant, LeBron James, Kevin Durant na Stephen Curry ambao wote kwa pamoja wana mashabiki milioni 187 wanaowafuatilia katika mitandao hiyo. Ronaldo anaweza kuwa ameshindwa tuzo ya Ballon d’Or na Lionel Messi lakini mshambuliaji huyo amempita kwa mbali Muargentia huyo ambaye ana mashabiki milioni 120.8 pekee katika mitandao ya kijamii.

No comments:

Post a Comment