Thursday, February 25, 2016

UCHAGUZI WA FIFA KAMA KAWA PAMOJA NA PINGAMIZI.


UCHAGUZI wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA unatarajiwa kuendelea kama ulivyopangwa kesho baada ya mgombea Prince Ali bin al-Hussein kushindwa kesi yake ya kutaka uchaguzi usimamishwe. Prince Ali mwenye umri wa miaka 40, alifungua kesi kutokana na kutofurahishwa na taratibu za upigaji kura zilivyo lakini Mahakama ya Kimataifa ya Michezo-CAS imetupilia mbali kesi hiyo. Mgombea huyo raia wa Jordan alikuwa akitaka uwazi zaidi katika vyumba vya kupigia kura ili kuhakikisha uchaguzi huo unakuwa wa huru na haki. Akihojiwa Prince Ali amesema amefanya kila analoweza na anajutia kwasababu mfumo ndio umewaangusha.

No comments:

Post a Comment