Monday, March 28, 2016

ARSENAL BADO INA NAFASI YA KUTWAA LIGI KUU - OZIL.

KIUNGO mahiri wa Arsenal, Mesut Ozil ana uhakika kikosi chao bado kiko katika mbio za kufukuzia taji la Ligi Kuu pamoja na kuwa nyuma ya vinara Leicester City kwa alama 11 huku wakiwa wamebaki na mechi nane za kucheza. Arsenal walikuwa wakiongoza ligi mwanzoni mwa mwaka huu lakini wameteleza mpaka nafasi ya tatu baada ya kushinda mechi tatu kati ya 10 za mwisho walizocheza. Pamoja na pengo kubwa lililopo, Ozil bado anaamini Arsenal wanaweza kuwafukuzia vinara hao ingawa amekiri kuwa hawapaswi kufanya makosa mengine zaidi kama wanataka kurejea kileleni. Akihojiwa akiwa katika majukumu ya kimataifa na Ujerumani, Ozil hadhani kama kuna kitu kinashindikana pamoja na kuwa michezo imebaki michache kwani Leicester bado ana kibarua cha kukutana na timu kubwa.

No comments:

Post a Comment