Monday, March 28, 2016

ISCO AWAZODOA JUVENTUS.

MSHAMBULIAJI wa Real Madrid, Isco amesisitiza anafuraha kuitumikia timu hiyo kufuatia tetesi zilizozagaa zikimhusisha na yeye kwenda Juventus. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania alikuwa akiripotiwa kuwindwa na mabingwa hao wa Serie A sambamba na nyota wa Paris Saint-Germain Edinson Cavani. Hata hivyo, akiwa amebakia na misimu miwili katika mkataba wake, Isco amesema hana mpango wa kuondoka Santiago Bernabeu katika kipindi cha karibuni. Isco aliongeza kuwa anafurahia kuwepo Madrid na anataka kumaliza mkataba wake mpaka mwisho halafu ndio ataona kitu atafanya baada ya hapo.

No comments:

Post a Comment