Monday, March 28, 2016

PELLEGRINI KUENDELEA KUBAKIA UINGEREZA.

MENEJA wa Manchester City anayeondoka, Manuel Pellegrini amedokeza kuwa anaweza kubakia katika Ligi Kuu msimu ujao kama akipata klabu ambayo itakuwa na mipango mizuri. Meneja huyo raia wa Chile nafasi yake inatarajiwa kuchukuliwa na Pep Guardiola majira ya kiangazi na amekuwa akihusishwa na kwenda katika vilabu kadhaa ikiwemo Valencia, Zenit St, Petersburg na Arsenal. Pellegrini amesema anaweza kubakia Uingereza sababu kubwa ikiwa ni fungu kubwa wanalopata klabu ambalo linaruhusu hata zile ndogo kama Leicester City nazo kushindania taji. Meneja huyo aliongeza kuwa klabu zote Uingereza zina fedha na mipango mizuri ndio maana kila meneja anapenda kuja kufundisha humo.

No comments:

Post a Comment