Sunday, March 27, 2016

BRENDAN RODGERS KURUDI SWANSEA.

MENEJA wa zamani wa Liverpool, Brendan Rodgers anatarajiwa kuchukua mikoba ya kuinoa Swansea City katika msimu ujao wa Ligi Kuu 2016-2017. Meneja huyo raia wa Ireland ya Kaskazini aliisaidia Swansea kupata daraja mwaka 2011 kabla ya kujiunga na Liverpool mwaka mmoja baadae na kuwaongoza kumalizika katika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi msimu 2013-2014. Miaka mitatu ya Rodgers katika Liverpool ilimalizika Octoba mwaka jana kufuatia matokeo mabovu na toka wakati huo aliamua kuchukua mapumziko. Francesco Guidolin ndio meneja wa muda wa Swansea kwasasa baada ya Garry Monk kuachia ngazi Desemba mwaka jana lakini taarifa zinadai kuwa Rodgers ndiye atakayepewa mikoba ya moja kwa moja kuinoa klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment