Sunday, March 27, 2016

MAN CITY YAKUBALIANA NA DORTMUND KWA AJILI YA KUMSAJILI GUNDOGAN.

KLABU ya Manchester City inadaiwa kukubali kutoa kitita cha paundi milioni 25 kwa ajili ya kumnasa nyota wa Borussia Dortmund Ilkay Gundogan. Meneja ajaye Pep Guardiola anaripotiwa kutaka kukijenga upya kikosi cha City ambapo anataka kukamilisha usajili wake pindi michuano ya Euro 2016 itakapoanza. Gundogan ambaye mkataba wake na Dortmund unatarajiwa kumalizika mwaka 2017, anategemewa kusajiliwa wa kwanza wakati mzungumzo ya nyota wa Juventus Paul Pogba yakianza tena pamoja na dau kubwa la Mfaransa huyo. Isco ambaye meneja wa sasa wa City alitaka kumsajili kutoka Malaga kabla ya Real Madrid hawajaingilia na Aymeric Laporte nao pia wametajwa kuwepo katika orodha ya City.

No comments:

Post a Comment