Sunday, March 27, 2016

LUKAKU MGUU NJE MGUU NDANI EVERTON.

MSHAMBULIAJI nyota wa Everton, Romelu Lukaku amezidi kuongeza uwezekano wa kuondoka katika klabu hiyo baada ya kukiri kuwa angependelea zaidi kucheza michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao. Baba wa nyota huyo aliwahi kuzungumza katika moja mahojiano yake ambapo alidai kuwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji atajiunga na aidha Manchester United au Bayern Munich mwishoni mwa msimu huu. Lukaku amesema hashangai kuona baba yake akizitaja timu anazozipenda lakini amedokeza kuwa anaweza kuondoka Goodison Park ili atafute timu inayoshiriki michuano ya hiyo mikubwa Ulaya kwa vilabu msimu ujao. Lukaku aliendelea kudai kuwa msimu ujao atatimiza miaka 23 na anadhani itakuwa vyema kama akicheza michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment