Monday, March 28, 2016

SEAMAN AWAONYA ARSENAL KUHUSU WENGER.

KIPA wa zamani wa Arsenal, David Seaman amesema klabu hiyo inapaswa kubaki na meneja Arsene Wenger kwasababu wanaweza kuhatarisha kupitia matatizo kama yaliyowakuta Manchester United kufuatia kuondoka meneja wao mzoefu Sir Alex Ferguson. Wenger amekuwa chini ya shinikizo baada ya kutolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Kombe la FA huku kukiwa na matumaini finyu ya kutwaa taji la Ligi Kuu kutokana na kuwa nyuma ya vinara Leicester City kwa alama 11. Hata hivyo, Seaman bado anaamini Wenger ndio kocha sahihi kwa klabu hiyo na kumuunga mkono kwa kila anachofanya. Seaman amesema kama Arsenal wakiamua kumtimua Wenger wanaweza kukumbwa na matatizo kama yaliyowakuta United wakati Ferguson alipoondoka.

No comments:

Post a Comment