Sunday, March 27, 2016

NILICHUKIA KUCHEZA WINGA NIKIWA UFARANSA - HENRY.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa, Thierry Henry amekiri alikuwa akichukizwa kupangwa kucheza winga katika kikosi cha nchi yake. Henry mwenye umri wa 38, ambaye alistaafu soka mwaka 2014, bado ameendelea kubakia mfungaji bora wa wakati wote katika klabu ya Arsenal na Ufaransa. Lakini pamoja na kuwa sehemu ya kikosi kilichotwaa Kombe la Dunia mwaka 1998 na michuano ya Ulaya miaka miwili baadae, Henry amekiri hakuwa akifurahia kucheza nje ya eneo. Henry amesema pamoja na kutofurahia lakini alikuwa akijitahidi kuzoea hali hiyo ili aweze kuisaidia timu.

No comments:

Post a Comment