Sunday, March 27, 2016

GOTZE KUMFUATA KLOPP KIANGAZI.

MCHEZAJI nyota wa Bayern Munich, Mario Gotze anadaiwa kuamua kuondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu na kwenda kujiunga na meneja wake wa zamani Jurgen Klopp katika klabu ya Liverpool. Nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani, ameshindwa kupata nafasi ya kudumu katika kikosi cha Bayern chini meneja anayeondoka Pep Guardiola baada ya kucheza mechi 12 pekee msimu huu. Inaripotiwa kuwa sasa Gotze ameamua kwenda kuungana na Klopp ambaye alicheza chini yake wakati akiinoa Borussia Dortmund na kufanikiwa kushinda mataji mawili ya Bundesliga. Gotze ambaye alibanisha mapema mwezi huu kuwa bado anawasiliana na Klopp kwa kutumia ujumbe mfupi, amebakisha miezi 12 katika mkataba wake na anadaiwa kuwa hataki kusaini mkataba mwingine.

No comments:

Post a Comment