Monday, April 25, 2016

GIGGS AFUATA NYAYO ZA FERGUSON.

MENEJA msaidizi wa Manchester United, Ryan Giggs ametunukiwa tuzo ya heshima ya Merit inayotolewa na Chama cha Wachezaji wa Kulipwa-PFA. Winga huyo wa zamani wa United, aliibuka rasmi Old Trafford miaka 25 iliyopita na kufanikiwa kushinda tuzo zote za PFA za mchezaji bora wa mwaka pamoja na chipukizi bora wa mwaka katika kipindi chake akicheza soka. Giggs anafuata nyayo za nguli wa United Sir Alex Ferguson, Sir Matty Busby na Sir Bobby Charlton ambao wote wamewahi kushinda tuzo hiyo. Akipokea tuzo hiyo Giggs aliwashukuru wale wote ambao wamekuwa karibu naye katika kipindi chote cha maisha yake ya soka.

No comments:

Post a Comment