Tuesday, May 24, 2016

AS VITA WATOLEWA LIGI YA MABINGWA AFRIKA.

KLABU ya AS Vita ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC imetolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kosa la kumchezesha mchezaji asiyeruhusiwa. Idrissa Traore alichezeshwa katika mzunguko wa awali pamoja na kuwa bdo kumaliza adhabu yake ya kutochza mechi nne wakati akiwa mchezaji wa Stade Malien. Nafasi ya Vita katika michuano hiyo sasa itachukuliwa na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini. Vita waliwaondoa Sundowns katika hatua ya timu 16 bora kwa bao la ugenini baada ya timu hizo kutoka sare ya jumla ya mabao 2-2 katika michezo miwili waliyokutana. Traore alitumikia mechi moja pekee katika adhabu yake hiyo wakati alipopangwa katika mchezo dhidi ya Mafunzo uliochezwa Februari mwaka huu.

No comments:

Post a Comment