Tuesday, May 24, 2016

GOTZE HAENDI LIVERPOOL.

MENEJA mpya na baba wa mshambuliaji nyota wa Bayern Munich, Mario Gotze amesema kijana wake hatakwenda Liverpool kama taarifa zilivyokuwa zimezagaa kona mbalimbali. Kwasasa nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 amesema anataka kuanza upya akiwa katika klabu hiyo yenye maskani Allianz Arena. Jana Gotze alisitisha mkataba wake na kampuni ya uwakala ya Sports Total ambayo pia inawawakilisha nyota wengine wakiwemo Toni Kroos, Marco Reus na Benedikt Howedes na kuamua shughuli zake ziwe zikisimamiwa na familia yake. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo, meneja wake huyo Jurgen Gotze amesema hafamu kuhusu taarifa hizo za kwenda Liverpool kwani amekuwa akizungumza na mwanae mara kwa mara lakini hajawahi kumwambia suala hilo.

No comments:

Post a Comment