Tuesday, May 24, 2016

RONALDO AWATOA HOFU MASHABIKI WA MADRID.

MSHAMBULIAJI nyota wa Real Madrid amewasisitizia mashabiki wa klabu hiyo kuwa hawana sababu ya kuhofu baada ya kuondoka mazoezini mapema leo kufuatia kukwatuliwa na Kiko Casilla. Madrid walikuwa mazoezini kuelekea mchezo wao wa Jumamosi hii katika Uwanja wa San Siro dhidi ya mahasimu wao wa jiji Atletico Madrid, wakati Ronaldo alipogongana na golikipa huyo kabla ya kunyanyuka na kuondoka akiwa anachechemea kabla ya mazoezi kumalizika. Hata hivyo, mshambuliaji huyo amewaondoa hofu mashabiki wa klabu hiyo akiwaambia wana habari kuwa yuko fiti kwa asilimia 100. Akihojiwa Ronaldo amesema tatizo linalomkabili sio kubwa na katika muda mchache atakuwa fiti tena.

No comments:

Post a Comment