Tuesday, May 24, 2016

DILI LA MOURINHO LANUKIA OLD TRAFFORD.

WAWAKILISHI wa Jose Mourinho wanatarajiwa kukutana na maofisa wa Manchester United leo ili kukamilisha taratibu za Mreno huyo kuwa meneja mpya wa klabu hiyo. Wakala wa Mourinho, Jorge Mendes amesafiri leo asubuhi kwenda jijini London na anatarajiwa kuongoza majadiliano hayo. Kuna hatihati ya taarifa kutotangazwa leo lakini uthibitisho kuwa Mourinho ndio atakuwa meneja ajaye wa klabu hiyo unategemewa kutangazwa baadae wiki hii. United ilimtimua meneja wake Louis van Gaal mwenye umri wa miaka 64 jana, ikiwa zimepita siku mbili baada ya kushinda taji la Kombe la FA.

No comments:

Post a Comment