Tuesday, May 24, 2016

UNITED YAJIPANGA KUMTENGENEA FUNGU NENE IBRAHIMOVIC.

KLABU ya Manchester United inadaiwa kuwa tayari kumtengea ofa nono Zlatan Ibrahimovic ili awe moja ya usajili muhimu wa Jose Mourinho katika kipindi hiki cha kiangazi. Nyota huyo wa kimataifa wa Sweden anatafuta klabu mpya baada ya kuondoka kwa mabingwa wa Ufaransa Paris Saint-Germain. Wakati mkongwe huyo akiwa tayari kukubali uhamisho wa kwenda kucheza Ligi Kuu ya Marekani-MLS ka dau kubwa, United inajipanga kumpa bonge la ofa ambalo linaweza kumshawishi kuahirisha kwenda Marekani. Inadaiwa kuwa Ibrahimovic anatafuta mkataba ambao utalingana sawa na mshahara wa euro 350,000 alizokuwa akipata PSG na United wako katika mchakato wa kuliwezesha hilo ili waweze kumshawishi kutua Old Trafford.

No comments:

Post a Comment