Tuesday, May 24, 2016

SANDRO KUONYESHWA MLANGO WA KUTOKEA BARCELONA.

KATIBU wa Ufundi wa Barcelona, Robert Fernandez amethibitisha Sandro hataitumikia klabu hiyo msimu ujao. Sandro amewatumikia mabingwa hao wa Hispania katika michezo 20 msimu huu lakini amefanikiwa kucheza mara mbili pekee mwaka huu baada ya kupata majeruhi. Fernandez alibainisha kuwa mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 20 alikuwa na machaguo mengi ya kuondoka msimu uliopita lakini alichagua kubakia huku Barcelona ikiwa imefungiwa kufanya usajili. Fernandez amesema wanamshukuru Sandro kwa uamuzi wake wa kubakia msimu uliopita lakini wameshindwa kumuongeza mkataba mwingine kutokana na tabia alizoonyesha.

No comments:

Post a Comment