Tuesday, May 17, 2016

CHELSEA, SPURS WALIMWA ADHABU NA FA.

CHAMA cha Soka cha Uingereza-FA kimezitoza faini klabu za Chelsea na Tottenham Hotspurs jumla ya paundi 600,000 jana kwa kushindwa kuwazuia wachezaji wake baada ya kuzuka ugomvi baina yao katika Uwanja wa Stamford Bridge wezi huu. Chelsea wao watalipa kiasi cha paundi 375,000 na Spurs paundi 225,000 baada ya klabu zote kukiri kuvunja sheria katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya mabao 2-2 Mei 2 mwaka huu. Katika mchezo huo Chelsea walitoka nyuma na kuzima ndoto za Spurs kufukuzia taji la Ligi Kuu kwa kurudisha mabao mawili waliyokuwa wamefungwa na kupelekea mchezo huo kumalizika kwa sare. Mapema Spurs wao walinyukwa fainali ya moja kwa moja ya paundi 25,000 kwa wachezaji wake tisa kupokea kadi za njano kutoka kwa mwamuzi Mike Clattenburg kwenye mchezo huo.

No comments:

Post a Comment