Tuesday, May 17, 2016

LEICESTER WAZUNGUKA NA KOMBE LAO MTAANI.

WATU wanaokadiriwa kuwa robo milioni wameandamana mitaani kwa lengo la kuipongeza klabu ya Leicester City iliyoibuka bingwa wa Ligi Kuu kwa mara ya kwanza katika historia yake ya miaka 132. Mistari miwili mikubwa pamoja na gari kubwa lililo wazi vilizunguka mji huo ulio katikati ya Uingereza. Meneja wa Leicester Muitaliano Claudio Ranieri ameiambia BBC kuwa mji mzima ulifurika watu waliokuwa wakiishangilia timu yao ambayo ilicheza kwa kujitolea sana. Leicester walipewa nafasi moja tu kati ya 5000 ya kushinda taji hilo la ligi mwanzoni mwa msimu.

No comments:

Post a Comment