Tuesday, May 17, 2016

FAINALI EUROPA LEAGUE: LIVERPOOL WATUA SALAMA BASEL TAYARI KUIVAA SEVILLA, ORIGI, HENDERSON NDANI.

MSHAMBULIAJI wa Liverpool, Divock Origi amesafiri na kikosi cha timu hiyo kuelekea Basel ka ajili ya mchezo wao wa fainali ya Europa League dhidi ya Sevilla utakaofanyika kesho. Origi alikuwa amepata majeruhi ya kifundo cha mguu katika mchezo dhidi ya Everton uliofanyika Aprili 20 mwaka huu lakini alidai kuwa matumaini ya kurejea kabla ya msimu kumalizika. Katika mchezo huo Daniel Sturridge ndio anayetarajiwa kuanza huku Christian Benteke pia akipewa nafasi hiyo na sasa taarifa zinadai Origi yuko fiti baada ya kufanya mazoezi na wenzake jana. 
Origi anaweza kuwa miongoni mwa wachezaji wa akiba sambamba na kiungo Jordan Henderson ambaye naye pia amesafiri kwenda Basel baada ya kurejea uwanjani katika sare ya bao 1-1 waliyopata Liverpool dhidi ya West Bromwich Albion. Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp ametamba kuwa kikosi chake kiko tayari kukabiliana na mabingwa watetezi wa michuano hiyo Sevilla ambao wanalitafuta kulichukua kwa mara ya tatu mfululizo.

No comments:

Post a Comment