Tuesday, May 17, 2016

WAKALA WA IBRAHIMOVIC ADAI MAN UNITED HAWAJATOA OFA YEYOTE.

WAKALA wa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic, amedai kuwa hakuna ofa yeyote ya mkataba iliyotolewa na Manchester United kwa mteja wake. Siku chache kabla ya Ibrahimovic hajacheza mechi yake ya mwisho akiwa na Paris saint-Germain-PSG vyombo vya habari nchini Ufaransa vilidai kuwa United tayari wamemtumia ofa ya mkataba wa mwaka mmoja nyota huyo. Lakini wakala wake Mino Raiola alikanusha taarifa hizo akidai kuwa wanahabari siku hizi wamekuwa wakijitengenezea habari wenyewe zisizokuwa na ukweli wowote. Ibrahimovic alithibitisha Ijumaa iliyopita kuwa ataondoka Parc des Princes na kusheherekea taji la ligi baada ya kucheza mechi yake ya mwisho siku moja baadae. Nyota huyo anatarajiwa kukamilisha kibarua chake PSG Jumamosi hii katika mchezo wa fainali ya Kombe la Ufaransa dhidi ya Marseille.

No comments:

Post a Comment