Tuesday, May 17, 2016

LALLANA AKANUSHA TAARIFA ZA KUTAKA KWENDA SPURS.

NYOTA wa Liverpool, Adam Lallana amesema ataendelea kubakia katika klabu hiyo pamoja na kuvuma kwa tetesi kuwa anaweza kuwindwa na Tottenham hotspurs. Lallana mwenye umri wa miaka 28 alisajiliwa Liverpool akitokea Southampton kwa kitita cha paundi milioni 25 mwaka 2014 na toka wakati huo amefanikiwa kucheza mechi 57 za ligi na kufunga mabao tisa. Gazeti la The Sun la Uingereza liliripoti kuwa meneja wa zamani wa Southampton Mauricio Pochettino ambaye kwasasa ndio anayeinoa Spurs anaweza kutaka kumleta Lallana White Hart Lane. Lakini hata hivyo, Lallana alikanusha tetesi hizo na kudai kuwa bado amebakisha mkataba wa miaka mitatu Liverpool na anafurahia kufanya kazi chini Jurgen Klopp. Akihojiwa Lallana amesema amekuwa na mahusiano mazuri na Pochettino nje ya uwanja kwasababu ni marafiki lakini kwasasa yuko katika klabu kubwa na hana mpango wowote wa kuondoka.

No comments:

Post a Comment