Tuesday, May 17, 2016

DEL BOSQUE ATAJA SILAHA ZAKE, AWAACHA KINA TORRES, CAZORLA, COSTA NA MATA.

MSHAMBULIAJI nyota wa Chelsea, Diego Costa ameachwa katika kikosi cha awali cha wachezaji 25 cha timu ya taifa ya Hispania kwa ajili ya michuano ya Euro 2016. Kocha wa timu hiyo Vicente del Bosque pia amewatema kiungo wa Manchester United Juan Mata na mashambuliaji wa zamani wa Liverpool na Chelsea ambaye kwasasa yuko Atletico Madrid Fernando Torres. Hispania ambao ni mabingwa watetezi wa taji hilo wamepangwa kundi D sambamba na timu za Croatia, Jamhuri ya Czech na Uturuki. 
Costa mwenye umri wa miaka 27 ambaye alikosa michezo miwili ya mwisho ya Chelsea kutokana na kusumbuliwa na msuli wa paja, ameifungia Hispania bao moja pekee katika mechi alizocheza. Beki wa Bayern Munich Javi Martinez na kiungo wa Arsenal Santi Cazorla ni miongoni mwa wachezaji wengine walioachwa katika kikosi hicho cha Del Bosque.

No comments:

Post a Comment