Thursday, May 19, 2016

OFISA WA EL MERREIKH ACHUNGUZWA NA CAF KUFUATIA MADAI YA KUMPIGA MWAMUZI.

SHIRIKISHO la Soka la Afrika-CAF linamfanyia uchunguzi ofisa wa klabu ya Al Merreikh ya Sudan, Hatim Mohamed Ahmed baada ya kunaswa akimpiga mwamuzi Eric Otogo-Castane wa Gabon usoni. Tukio hilo lilitokea katika dakika ya 84 ya mchezo wa jana wa Kombe la Shirikisho kati ya Merreikh na Kawkab Marrakech ya Morocco. CAF inalifanyia uchunguzi kwa karibu tukio hilo huku wakisubiri ripoti ya waamuzi. Kawkab walishinda mchezo huo kwa mabao 2-0 ambayo yote yalifungwa kwa njia ya panati na kuwafanya kusonga mbele kwa jumla ya mabao 2-1.


No comments:

Post a Comment