Friday, May 20, 2016

CHELSEA WATAKA KUMSAJILI LUKAKU.

KLABU ya Chelsea inadaiwa kutaka kumsajili tena mshambuliaji wao wa zamani Romelu Lukaku kutoka klabu ya Everton. Chelsea walimuuza Lukaku kwa kitita cha paundi milioni 28 kwenda Everton mwaka 2014, baada ya kuitumikia timu hiyo kwa mkopo na toka wakati huo nyota huyo amefunga mabao 61 katika mechi 127 alizocheza. Chelsea sasa wanadaiwa kutaka kumrejesha tena mshambuliaji huyo ingawa inadaiwa Everton watataka kulipwa ada ya paundi milioni 61 kiasi ambacho kinadaiwa kitaweza kulipwa. Chelsea pia inawawinda nyota wa Napoli Gonzalo Higuain na mshambuliaji wa Juventus Alvaro Morata ili kuimarisha safu yao ya ushambuliaji.

No comments:

Post a Comment