Friday, May 20, 2016

SUAREZ ADAI HAKUTEGEMEA KAMA ATAWEZA KUCHUKUA NAFASI YA MESSI.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Luis Suarez amesema hakutegemea kuchukua nafasi ya Lionel Messi ya mshambuliaji kiongozi kama alivyofanya msimu huu. Suarez amekuwa akiimarika toa ajiunge na Barcelona akitokea Liverpool na amefanikiwa kuisaidia timu hiyo kutwaa taji la La Liga mara mbili huku mwenyewe akimaliza kama mfungaji kinara. Suarez amefunga mabao 40 katika mechi 35 za ligi alizocheza msimu huu na kumzidi mshambuliaji nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo katika tuzo ya Pichichi kwa kufunga hat-trick katika mchezo wao mwisho wa msimu. Kwasasa Messi ambaye ni mshindi wa tuzo tano za Ballon d’Or amerudi nyuma na kushambulia akitokea upande wa kushoto ili kumpisha Suarez nafasi ya katikati. Akihojiwa Suarez amesema hakutegemea kucheza nafasi hiyo kwani ndio ilikuwa ikitumiwa na Messi lakini wamekuwa wakielewana vyema ndani na nje ya uwanja.

No comments:

Post a Comment