Friday, May 20, 2016

GOTZE ASHAURIWA KUONDOKA BAYERN.

KOCHA wa timu ya taifa ya Ujerumani, Joachim Loew amemshauri Mario Gotze kuondoka Bayern Munich ili kupiga hatua zaidi katika soka lake. Gotze mwenye umri wa miaka 23 anakaribia kumaliza mkataba wake na Bayern na amekuwa akihusishwa na tetesi za kuondoka Allianz Arena kiangazi hiki. Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani ameshindw akupata nafasi katika kikosi cha kwanza cha Bayern katika kipindi cha miaka mitatu toka ajiunge nao akitokea Borussia Dortmund. Akihojiwa Loew amesema Gotze ni mchezaji mzuri na hana shaka na uwezo wake lakini anadhani uhamisho unaweza kumletea changamoto mpya na kumfanya kuimarika zaidi ya alivyo sasa.

No comments:

Post a Comment