Friday, May 20, 2016

OZIL NDIO MCHEZAJI BORA WA MWAKA WA ARSENAL.

KIUNGO wa mahiri wa kimataifa wa Ujerumani, Mesut Ozil amechaguliwa na mashabiki kuwa mchezaji bora wa mwaka wa Arsenal kutokana na kiwango cha juu alichoonyesha msimu huu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 ameshinda tuzo hiyo akiwazidi Alexis Sanchez aliyeshika nafasi ya pili na Hector Bellerin aliyeshika nafasi ya tatu. Ozil amekuwa katika kiwango kizuri akifunga mabao nane na kutengeneza nafasi zingine 181 msimu huu ambazo zimechagiza kwa kiasi kikubwa Arsenal kumaliza katika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Leicester City. Kiwango hicho pia kilimfanya Ozil kuteuliwa katika orodha ya tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa PFA ambayo ilinyakuliwa na Riyad Mahrez wa Leicester.

No comments:

Post a Comment