Thursday, May 19, 2016

MABINGWA LEICESTER KUONGEZA WATATU KIANGAZI.


MAKAMU mwenyekiti wa Leicester City, Aiyawatt Srivaddhanaprabha amedai klabu hiyo inatarajia kusajili wachezaji watatu au wanne katika kipindi cha usajili wa majira ya kiangazi ili waweze kujiimarisha kwa ajili ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Ubingwa Ligi Kuu uliwafanya Leicester kupata tiketi ya kushiriki michuano hiyo msimu uja ikiwa ni mara yao ya kwanza. Leicester pia watashiriki michuano ya Kombe la Kimataifa litakalofanyika kipindi hiki cha kiangazi na wanatajia kupambana na bingwa wa Kombe la FA katika mchezo wa Ngao Hisani. Akizungumza wakiwa nchini Bangkok walipokwenda kwa ziara makamu mwenyekiti huyo amesema wanafurahia kikosi walichonacho hivi sasa lakini msimu ujao wana mashindano mengi zaidi hivyo inabidi waongeze baadhi ya wachezaji ili kujiimarisha.

No comments:

Post a Comment