Monday, May 16, 2016

WALCOTT AJIBU KUFUATIA KUACHWA KWAKE KATIKA KIKOSI CHA UINGEREZA.

WINGA wa Arsenal, Theo Walcott amejibu kuachwa kwake katika kikosi cha timu ya taifa ya Uingereza kwa ajili ya michuano ya Euro 2016, akisisitiza kuwa wakati akisononeshwa na hilo lakini amekubali uamuzi wa meneja Roy Hodgson. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 amekuwa akihangaika kupata nafasi katika kikosi cha kwanza mwishoni mwa kampeni za msimu wa 2015-2016 akiwa hajapata nafasi ya kuanza katika mechi yeyote ya Ligi Kuu toka Februari 28. Mara ya mwisho kuifungia Arsenal bao ilikuwa ni Aprili wakati waliposhinda mabao 4-0 na kufuatia kuachwa huko na Hodgson, Walcott amekubaliana na uamuzi huo na kuitakia timu kila la heri katika michuano hiyo itakayofanyika Ufaransa. Walcott alituma ujumbe katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter akidai kusikitishwa kwake kuachwa kwenye kikosi hicho lakini akikubaliana na uamuzi wa Hodgson.

No comments:

Post a Comment