Sunday, June 26, 2016

BREXIT ITAATHIRI LIGI KUU - FABREGAS.

KIUNGO mahiri wa kimataifa wa Hispania na klabu ya Chelsea, Cesc Fabregas ameelezea kujitoa kwa Uingereza katika Umoja wa Ulaya-EU kama kitendo cha makosa na kinaweza kuja kusababisha matatizo mengi. Fabregas mwenye umri wa miaka 29, ametumia mud wake wa kucheza soka katika Ligi Kuu akianzia Arsenal ambako alicheza kuanzia mwaka 2003 mpaka 2011 na sasa Chelsea ambao alijiunga nao akitokea Barcelona mwaka 2014. Nyota huyo anaamini kuwa uamuzi huo hautaathiri uchumi na maisha ya kila ya kila nchini huko lakini pia itakuwa na athari kubwa katika soka na uwezo wa kusajili wachezaji. Akihojiwa Fabregas amesema amesikitishwa na uamuzi huo kwani binafsi anaona ni makosa na kitu ambacho hakukitegemea Uingereza kujitenga. Nyota huyo aliongeza uamuzi huo utaathiri Ligi Kuu, itakuwa vigumu kusajili wachezaji na mishahara itabadilika kama paundi itakaribiana na euro.

No comments:

Post a Comment