Sunday, June 26, 2016

ZIDANE ADOKEZA MADRID KUMUWANIA POGBA.

MENEJA wa Real Madrid, Zinedine Zidane amedokeza kuwa klabu hiyo inaweza kumuwania Paul Pogba kufuatia michuano ya Ulaya inayoendelea nchini Ufaransa. Zidane mara kadhaa ameshakaririw akieleza jinsi anavyomhusudu Pogba, na wakala wa nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa, Mino Raiola amesema hivi karibuni kuwa mazungumzo ya awali yameshaanza na Juventus kwa ajili ya uhamisho wake. Akihojiwa kuhusiana na suala hilo, Zidane alikataa kuingia kwa ungani akidai kuwa kwasasa bado lakini katika kipindi cha wiki mbili zijazo itajulikana. Kwa upande mwingine, kuna taarifa kuwa James Rodriquez anatarajia kukutana na Zidane ili kujadili mustakabali wake huku ikitarajiwa matokeo ya mazungumzo yao yanaweza kupelekea mchezaji huyo kuondoka. Rodriquez amekuwa katika rada za Manchester United, lakini anatarajiwa kuchelewa kurejea Madrid baada ya kushiriki michuano ya Copa America ambapo Colombia imemaliza katika nafasi ya tatu.

No comments:

Post a Comment