Saturday, June 25, 2016

BREXIT YAMUWEKA BALE NJIA PANDA.

WAKILI mmoja wa masuala ya michezo, amedai kuwa hadhi ya Gareth Bale inaweza kuwa katika tishio kwasababu ya uamuzi wa Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya-EU. Timu za Hispania ni miongoni mwa timu ambazo zina viwango maalumu kwa wachezaji wanaotoka nje ya EU, kitu ambacho nyota huyo wa kimataifa wa Wales anaweza kuwa Uingereza ikijenga rasmi na umoja huo. Kwasasa Madrid ni kama wamepita kiwango cha zaidi ya wachezaji watatu wanaotoka nje ya EU kwasababu ya kuwa na James Rodriquez, Danilo, Casemiro na Bale, lakini taarifa zinadai kuwa taratibu za kujitoa huko zinaweza kuchukua miaka miwili mpaka saba. Kama Bale akiendelea kuwepo Madrid mpaka Uingereza itakapojitenga rasmi ni wazi kuwa atahesabika kama mchezaji anayetoka nje ya EU hivyo klabu hiyo italazimika kupunguza mchezaji mmoja.

No comments:

Post a Comment