Saturday, June 25, 2016

FIFA YAINGILIA KATI MGOGORO WA SOKA ARGENTINA.

SHIRIKISHO la Soka Duniani-FIFA limesema limetwaa madaraka ya Shirikisho la Soka la Argentina kutoka kwa uongozi wa sasa na watasaidia kuteua jopo la dharura litakaloweza kushughulikia mambo yake. FIFA ilitangaza uamuzi huo jana, siku mbili kabla ya Lionel Messi hajaiongoza Argentina kucheza fainali ya michuano ya Copa America dhidi ya Chile huko Rutherford, New Jersey. Alhamisi rais wa shirikisho hilo, Luis Segura ambaye pia ni mjumbe ya baraza la FIFA, alishitakiwa kwa kosa ufisadi kuhusiana na haki za matangazo ya luninga. Wakiongozwa na Julio Grondona toka miaka ya sabini, shirikisho hilo limekuwa katika migogoro toka alipofariki makamu huyo wa rais wa FIFA mwaka 2014. Taarifa ya FIFA imedai kuwa kamati maalumu ya kuweka mambo sawa itakayokuwa na wajumbe wasiozidi saba ndio itakayopewa jukumu la kuongoza shughuli za kila siku za shirikisho hilo. Uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika Julai 2017.

No comments:

Post a Comment