Saturday, June 25, 2016

MAKUNDI YA KUFUZU KOMBE LA DUNIA AFRIKA HADHARANI.

TIMU tatu kati ya tano za Afrika zilizoshiriki michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014 zimepangwa katika kundi moja katika mechi za kufuzu michuano hiyo mwaka 2018. Timu moja kati ya Algeria, Cameroon na Nigeria ndio zitaweza kushiriki michuano hiyo ya Urusi baada ya Shirikisho la Soka la Afrika-CAF kupanga ratiba ya makundi matano ta kufuzu jana. Timu hizo tatu zenye nguvu kisoka barani Afrika zimepangwa na Zambia. Ni mshindi mmoja pekee katika makundi hayo matano ndio atafuzu michuano hiyo itakayoshirikisha timu 32. Ivory Coast ambao watakuwa wakitafuta nafasi ya kufuzu michuano hiyo kw amara ya nne, wamepangwa kundi moja na Gabon, Mali na Morocco. Mechi hizo za makundi zinatarajiwa kuanza kutimua vumbi Octoba mwaka huu na kuendelea mpaka Novemba mwaka 2017.

Makundi hayo ni
Kundi A: Tunisia, Libya, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, Guinea.
Kundi B: Zambia, Cameroon, Algeria, Nigeria
Kundi C: Gabon, Mali, Ivory Coast, Morocco
Kundi D: Senegal, Afrika Kusini, Burkina Faso, Cape Verde
Kundi E: Ghana, Misri, Congo, Uganda

No comments:

Post a Comment