Saturday, June 25, 2016

MORATA BADO KIPUSA LIGI KUU.

WAKALA wa mshambuliaji Alvaro Morata, Juanna Lopez amedai kuwa bado mteja wake amepata ofa kutoka klabu kubwa Ligi Kuu. Ilithibitishwa Jumatano iliyopita kuwa Morata mwenye umri wa miaka 23, atarejea Real Madrid kutoka Juventus kama makubaliano yalivyokuwa. Lakini Lopez amedokeza kuwa mustakabali wa mteja wake unaweza usiwe Santiago Bernabeu chini Zinedine Zidane na kuongeza tetesi kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Hispania anaweza kuuzwa na Madrid kwa faida. Akihojiwa Lopez amesema Morata bado ana ofa kutoka klabu kubwa Ligi Kuu, hivyo wanasubiri kuona iakavyokuwa baada ya kuzungumza na Zidane.

No comments:

Post a Comment