Monday, June 20, 2016

INTER YAPANIA KUMNASA YAYA TOURE.

KLABU ya Inter Milan imepania kumsajili kiungo mkongwe wa kimataifa wa Ivory Coast na klabu ya Manchester City Yaya Toure. Toure mwenye umri wa miaka 33, kwasasa amebakisha mwaka mmoja katika mkataba wake kwenye klabu hiyo yenye maskani yake katika Uwanja wa Etihad. Kiungo huyo aliuzwa kwa City wakati huyo ikiongozwa na meneja wa sasa wa Inter Milan Roberto Mancini, kwa kitita cha paundi milioni 24 na Pep Guardiola mwaka 2010 wakati wawili hao walipokuwa wote Barcelona. Hakuna makubaliano yeyote yaliyoafikiwa lakini tetesi zinadai kuwa kuna nafasi ya asilimia 50 kama usajili utafanyika.

No comments:

Post a Comment