Monday, June 20, 2016

SHABIKI WA RONALDO AIPONZA URENO.

SHIRIKISHO la Soka la Ulaya-UEFA limetangaza kuwa shabiki wa Ureno aliyeingia uwanjani na kwenda kupiga picha na Cristiano Ronaldo anaweza kulipnza Shirikisho la Soka la nchi hiyo kutozwa faini. UEFA imedai kuwa imefungua kesi ya kinidhamu dhidi ya shirikisho hilo kwa kosa la uvamizi wa uwanja. UEFA huwa inazichukulia hatua timu za taifa ambazo zinashindwa kuwadhibiti mashabiki wake uwanjani. Katika tkio hlo shabiki mmoja alikimbia uwanjani katika mchezo uliomalizika kwa sare ya bila kufungana kati ya Ureno na Austria Jumamosi iliyopita, kabla ya Ronaldo kuwapa ishara ya kuamuacha kwa watu wa usalama waliojaribu kumzuia.

No comments:

Post a Comment