Monday, June 20, 2016

WENGER KUSAJILI WATATU TU KIANGAZI.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema hataweza kununua wachezaji zaidi ya watatu katika kipindi cha usajili wa kiangazi kwani inaweza kukiyumbisha kikosi chake. Klabu hiyo mpaka sasa tayari wamemsajili kiungo Granit Xhaka kutoka Borussia Monchengladbach na Wenger alikuwa na matumaini ya kumfanya Jamie Vardy kuwa usajili wake wa pili katika kipindi hiki. Lakini akihojiwa hivi karibuni Wenger alidai kuwa anategemea mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Uingereza kukataa ofa yao na kuamuai kubakia Leicester City. Katika mahojiano hayohayo, Wenger alieleza mikakati yake kuwa hana kufanya mabadiliko makubwa sana katika kikosi chake lakini bado anaangalia baadhi ya wachezaji ambao ataweza kuwanunua. Wenger amesema baada ya kupata kiungo Xhaka bado wataendelea kutafuta wachezaji wengine mmoja au wawili lakini haitakuwa kazi rahisi.

No comments:

Post a Comment