Monday, June 20, 2016

SPURS YAKUBALI KUTOA PAUNDI MILIONI 11 KWA AJILI YA WANYAMA.

KLABU ya Tottenham Hotspurs inadaiwa kukubali kutoa ada ya paundi milioni 11 ka ajili ya kumnasa kiungo wa Southampton Victor Wanyama. Inadaiwa kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Kenya mwenye umri wa miaka 24, ambaye alijiunga na Southampton kwa kitita cha paundi milioni 12.5 kutokea Celtic Julaia mwaka 2013, anafanyiwa vipimo vya afya katika klabu hiyo White Hart Lane. Uhamisho huo utamfanya Wanyama kuungana na kocha wake wa zamani ambaye ndio aliyemtoa Celtic Mauricio Pochettino. Wanyama aliomba kuondoka kiangazi mwaka jana baada ya Tottenham Hotspurs kuonyesha nia ya kumtaka lakini alibakia St. Mary’s na kuisaidia Southampton kumaliza katika nafasi ya sita katika msimamo wa Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment