Thursday, June 16, 2016

KAKA YAKE KROOS ADAI NDUGUYE ANA THAMANI YA PAUNDI MILIONI 95 PAMOJA NA POGBA.

KAKA yake Toni Kroos aitwaye Felix amedai kuwa kiungo huyo wa Real Madrid ana thamani ya paundi milioni 95 pamoja na kiungo wa Juventus Paul Pogba kwakuwa ndio mchezo bora duniani kwasasa kwenye nafasi hiyo. Felix mwenye umri wa miaka 25 anayekipiga katika klabu ya Union Berlin ametoa kauli hiyo kujibu taarifa za Madrid kumtoa kaka yake kama ofa pamoja na fedha kwa ajili ya kumnasa Pogba mwenye umri wa miaka 23. Toni Kroos mwenye umro wa miaka 26 ambaye amecheza mechi 44 za mashindano yote akiwa na Madrid msimu uliopita, amefunga bao moja wakati Pogba aliyechezea Juventus mechi 49 amefunga mabao 10 na kuisaidia timu yake hiyo kutwaa taji la Serie A kwa mara ya nne mfululizo. Akihojiwa Felix amesema ameshangazwa na taarifa za Madrid kutoa fedha kwa ajili ya Pogba pamoja na ofa ya kaka kwani anadhani jambo linapaswa kufanya kinyume chake kutokana na ubora mkubwa alionao nduguye huyo. Felix aliendelea kudai kuwa anadhani Juventus ndio wanapaswa kutoa kiasi hicho cha paundi milioni 45 pamoja na Pogba ili waweze kumnasa Toni.

No comments:

Post a Comment