Sunday, June 26, 2016

KOCHA WA URUSI AJIUZULU.

KOCHA wa timu ya taifa ya Urusi, Leonid Slutsky amejiuzulu rasmi nafasi hiyo kufuatia kufanya vibaya kwa nchi hiyo katika michuano ya Ulaya inayoendelea nchini Ufaransa. Kocha huyo wa CSKA Moscow sasa atahamishia nguvu zake katika klabu yake, baada ya kuchuka kibarua cha timu ya taifa Agosti mwaka jana baada ya kutimuliwa kwa Fabio Capello. Baada ya kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Wales, Slutsky amesema kikosi hicho kinahitaji kocha mwingine na sasa Shirikisho la Soka la nchi hiyo-RFS limethibitisha kuondoka kwake. Rais wa RFS, Vitaly Mutko alimshukuru Slutsky kwa kazi aliyofanya kwa kipindi chote walichokuwa naye na kudai kuwa aliikuta timu hiyo katika kipindi kigumu wakati ambapo walikuwa hawana hata matumaini ya kufuzu micuano ya Ulaya. Mutko aliongeza kuwa kilichotokea Ufaransa kimesababishwa na mambo mengi ambayo hataki kuyazungumzia lakini kwa mwazo yake Slutsky alifanya kazi yake vyema.


No comments:

Post a Comment