Sunday, June 26, 2016

SWANSEA LANASA BEKI LA AJAX.

BEKI Mike van der Hoorn amedai anatarajia kusafiri kuelekea Wales wiki hii kwa ajili ya makubaliano binafsi na Swansea City baada ya klabu hiyo kukubalia kulipa euro milioni 2.5 kwa uhamisho wake kutoka Ajax Amsterdam ya Uholanzi. Van der Hoorn amesema atafanya majadiliano yeye mwenyewe kuhusiana na mshahara wake na bakshishi baada ya makubaliao kati ya klabu hizo mbili kuafikiwa. Akihojiwa beki huyo amesema amefurahi kupata nafasi ya kucheza katika Ligi Kuu hususani katika klabu kubwa kama Swansea. Van der Hoorn mwenye umri wa miaka 23, ni mchezaji wa zamani wa kikosi cha timu ya taifa ya Uholanzi kwa vijana chini ya umri wa miaka 21, aliyeigharimu Ajax euro milioni nne kumuhamisha kutoka Utrecht miaka mitatu iliyopita.

No comments:

Post a Comment