Saturday, June 25, 2016

LIVERPOOL WAONGOZA MBIO ZA KUMNASA SADIO MANE.

TAARIFA zinadai kuwa Liverpool wanazidi kuwa na uhakika wa kumnasa mshambuliaji wa Southampton Sadio Mane. Liverpool imekuwa katika mzungumzo na Southmpton kwa muda mrefu sasa wakijaribu kushawishi kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Senegal na taarifa zilizotoka karibuni zinadai kuwa klabu hiyo inakaribia kufanikiwa suala hilo. Meneja wa Liverpool, Jurgen Klopp amemtaja Mane kama moja ya vipaumbele vyake wakati akijaribu kuimarisha kiksoi chake kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu. Mane alimkuna Klopp wakati timu hizo zilipokutana katika mechi za Ligi Kuu wakati alipofunga katika mchezo wa sare ya bao 1-1 uliofanyika Anfield na ule aliofunga mabao mawili na kuipa Southmpton ushindi wa mabao 3-2 katika Uwanja wa St, Mary’s. Manchester United na Manchester nazo pia zimekuwa zikimuwania mane lakini Liverpool wamepania kushinda mbio hizo.

No comments:

Post a Comment