Saturday, June 25, 2016

MESSI AKIRI KUKOSEA KUIKOSOA AFA KIPINDI HIKI.

MSHAMBULIAJI nyota wa Argentina, Lionel Messi amekiri kufanya makosa kwa kauli yake ya kuponda Shirikisho la Soka la nchi yake-AFA, lakini amekataa kutumia hali hiyo kama sababu ya kushindwa mchezo wa fainali ya Copa America dhidi ya Chile kesho. Nyota huyo wa Barcelona aliweka wazi hisia zake kuhusu AFA Alhamisi iliyopita wakati alipotuma picha katika mitandao wa kijamii huku kukiwa na Ujumbe mkali wa kuiponda AFA. Nahodha huyo wa Argentina amekiri kufanya kosa kwa kutuma huo lakini ni kwasababu tu wanakabiliwa na mchezo wa fainali. Messi amesema anafahamu hakupaswa kutoa kauli hiyo kwasababu mchezo wao fainali uko karibu lakini ni wazi shirikisho lao linapswa kujipanga na kuweka mambo yake sawa. Argentina itakuwa ikifukizia taji lake la kwanza michuano hiyo toka mwaka 1993 baada ya mwaka jana pia kulikosa kwa kufungwa na Chile kwa changamoto ya mikwaju ya penati.

No comments:

Post a Comment